Text Widget

Recent Posts

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SIASA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SIASA. Onyesha machapisho yote

Julai 12, 2014

Wakurd wazozana na Waziri Mkuu Nouri Al Maliki


Massoud Barzani, kiongozi wa Iraq Kurdistan
Ugomvi wa kisiasa baina ya jimbo la Iraq la Kurdistan na eneo lilobaki la Iraq, umezidi kuwa mkali.
Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Iraq, Hoshyar Zebari, mwanasiasa maarufu kabisa wa Kikurd katika serikali ya Iraq, ameiambia BBC kwamba Waziri Mkuu Nouri Al Maliki lazima aombe msamaha na abadilishe kauli yake kuhusu Kurdistan.

TAZAMA UKATILI HUU:MTOTO AFICHWA UVUNGUNI KWA MIAKA 6 MOROGORO



Wakati jamii ikiwa bado haijasahau mateso aliyoyapata mtoto Nasra Mvungi na kusababisha  kifo chake, tukio lingine la aina hiyo limetokea katika Kijiji cha Matongola, Tarafa ya Magole Wilaya ya Kilosa, baada ya kubainika mtoto wa miaka sita akiwa amefichwa uvunguni mwa kitanda na kufanyiwa vitendo vya kikatili na mama yake mzazi. 

Juni 22, 2014

BREAKING NEWS!!! DALADALA ZA GONGANA NA KUUWA WATU 19 DAR LEO HII.


TAHADARI PICHA ZINA TISHA
 Habari zilizo tufikia ni kwamba ajali hii mbaya imetokea eneo la Makongo. Coaster mbili zimegongana watu 20 wamefariki hapo hapo. 
Moja wapo ya Daladala aina ya Coster iliyo husika katika ajali hiyo

Juni 16, 2014

Habari Picha:  zilizochapishwa za mauaji Iraq.

mauaji1
Vuguvugu la Sunni lenye msimamo mkali la ISIS ambalo limeteka maeneo ya Kaskazini mwa Iraq limesambaza picha ambazo zinaonyesha jinsi wapiganaji wake walivyoangamiza idadi kubwa ya wanajeshi wa Iraq.
mauaji2Kwa mujibu wa BBC, Picha zinazosambazwa kupitia internet zinaonyesha miili ya watu iliyosongamana ndani ya mtaro ikiwa imepelekwa hapo kwa kutumia malori.

Habari Mbaya Kutoka Kenya,Watu 48 wauawa Usiku wa Kuamkia leo

Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Kiislamu wameshambulia kituo cha polisi na mahoteli na vijiji mjini Mpeketoni, pwani ya Kenya .
Makabiliano makali yameripotiwa sehemu kubwa ya Jumapili usiku huku wakaazi wakitorokea maeneo ya msitu karibu na kisiwa cha Lamu..

Juni 10, 2014

TAZAMA PICHA NA HABARI:WAZIRI WA NISHATI NA MADINI WATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA, WASHINGON, DC‏

Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akitambulisha Mhe. Waziri wa Nishati na Madini Prof Sospeter Muhongo kwa Mkuu wa Utawala na Fedha wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, Mama Lily Munanka siku ya Jumatatu June 9, 2014 Waziri wa Nishati na Madini na ujumbe wake walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani ulipo mtaa wa 22, jijini Washington, DC.

Juni 09, 2014

Hiki ndicho Kilichosemwa bungeni juu ya picha chafu zinazosambazwa mitandaoni za watu maarufu.




 
bungeeSakata la kusambaa picha zisizokuwa na maadili mitandaoni zikiwemo za watu maarufu hapa nchini leo limezungumziwa tena katika bunge la Tanzania kule Dodoma ambapo katika kipindi cha maswali na majibu Mhe. Habib Mnyaa ameonekana akihoji serikali inachukua hatua gani juu ya watu wanaotuma picha zao

Mei 27, 2014

HABARI PICHA:POLISI WAUA TENA MAJAMBAZI TEMEKE




Mwili wa mmoja wa majambazi ukiwa chumba cha kuhifadhia maiti 


Mwili wa jambazi mwingine ukiwa umeharibika vibaya baada ya kipigo kikali kutoka kwa wananchi wenye hasira.


Mei 26, 2014

HII NI TAARIFA KUHUSU JESHI LA NIGERIA KUBAINI WALIKOFICHWA WASICHANA WALIOTEKWA



Screen Shot 2014-05-27 at 12.31.00 AM
Jeshi la nchini Nigeria limesema linajua mahali walikofichwa zaidi ya wasichana 200 waliotekwa wakiwa shuleni lakini hawawezi kuitaja sehemu hiyo hadharani.
Wasichana hao walitekwa na kundi la kigaidi la Boko Haram ambalo linadai haliwezi kuwaachia hadi watakapobadilishana wafungwa wao na serikali ya nchi hiyo.

MBEYA CITY WACHAPWA 2-1 NA FC LEOPARD


Mbeya City Usiku huu imefungwa Bao 2-1 na AFC Leopards ya Kenya katika Mechi yao ya Pili ya KUNDI B la Mashindano ya CECAFA NILE BASIN CUP iliyochezwa huko Khartoum, Sudan.
Hadi Mapumziko, Mbeya City walikuwa nyuma kwa Bao 2-0 zilizofungwa na Mudde Musa katika Dakika ya 30 na Were Paul, Dakika ya 35.
Bao la Mbeya City lilifungwa na Deus Kaseke katika Dakika za Majeruhi.
Kwenye Mechi ya Kwanza, Mbeya City waliifunga Academie Tchite ya Burundi Bao 3-2 na Mechi yao ya mwisho ya KUNDI B ni hapo Jumatano dhidi ya Enticelles ya Rwanda.

KUTOKA IRINGA MJINI:CHADEMA WATIMULIWA KATIKA MAZISHI YA DEREVA BODA BODA , WASEMA WAO SI CHAMA CHA SIASA


Waombolezaji wakitoa heshima  zao huku wengine wakichukua picha za kumbukumbu 

Mei 21, 2014

Soma hili:Tapeli Sugu akamatwa Nje ya Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma,Huyu hapa.


Tapeli Sugu aliyejulikana kwa Jina la Ally Mwinyi Kutoka Vikindu-Pwani aliyekamatwa Parking za Madreva wa Wabunge-Dodoma akiwa chini ya Ulinzi tayari kwa Kupelekwa Kituo cha Polisi kwa hatua za Kisheria.

Mei 20, 2014

Picha Kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Kimataifa:fanyakazi Hodari wa Wizara na Wafanyakazi Bora wapokea vyeti vyao


 Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw. Batholomeo Jungu.
 Katibu Mkuu akimkabidhi Cheti Mfanyakazi Bora wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu,

Januari 20, 2014

HATIMAYE BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI LATANGAZWA....UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI WAPYA..SOMA ZAIDI HAPA

Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue.

Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue ametangaza baraza jipya la mawaziri wakiwemo walioziba nafasi tano zilizokuwa wazi na wengine kuhamishiwa wizara nyingine!

Januari 09, 2014

NDESAMBURO AWANG'AKIA MAMLUKI WA CHADEMA.


MBUNGE wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), amesema matatizo yanayokikumba chama hicho kwa sasa yanatokana na kundi la watu wachache wenye uchu wa madaraka, ambao pia wanatumiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Desemba 18, 2013

TAZAMA TZ KAMA KENYA: ABIRIA YOYOTE ATAKAYE KUTWA AMESIMAMA KWENYE DALADALA KUTOZWA FAIN...!!!,"SOMA HAPA ZAIDI"

POLISI Kikosi cha Usalama Barabarani, inaandaa sheria itakayosaidia kudhibiti ujazaji wa watu kwenye magari ya abiria, ambayo abiria atakayekutwa amesimama, atatozwa faini.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Desemba 09, 2013

MABOMU YALINDIMA MKUTANO WA DR SLAA KIGOMA,"SOMA HAPA ZAIDI"

JESHI la Polisi wilayani Kasulu mkoani Kigoma, jana lililazimika kutumia mabomu ya machozi ili kumnusuru Katibu Mkuu wa Chama cha 
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa asifanyiwe fujo. Habari za uhakika kutoka Kasulu zinasema, Dk. Slaa alijikuta katika wakati mgumu baada ya kundi la vijana wanaokadiriwa kuwa kumi wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali kuzua fujo.

Desemba 06, 2013

TAZAMA MAZISHI YA NELSON MANDELA KUVUNJA REKODI,"SOMA ZAIDI HAPA"

Na Mwandishi wetu,mwananchi
 0
Sh


Afrika na dunia inatarajiwa kushuhudia kitu kipya katika maziko ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela (95) aliyefariki dunia juzi, baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi sita.
Serikali ya Afrika Kusini imesema kiongozi huyo ambaye atazikwa Desemba 15, imeandaa mazishi ya kihistoria yanayosemekana yatazidi yale ya Papa John 11.
Matukio ya shughuli mbalimbali zinazohusu mipango ya maziko ya kiongozi huyo maarufu yanatarajiwa kushuhudiwa sehemu mbalimbali duniani, tofauti na tukio jingine lililowahi kutokea barani Afrika mbali na kombe la dunia.
Rais Jacob Zuma alisema jana kwamba “Mpendwa wetu Madiba atazikwa kwa heshima zote za Serikali. Nimeagiza bendera zote za Afrika Kusini zipepee nusu mlingoti na hiyo itaendelea hivyo hadi tutakapokamilisha mazishi yake.
Mazishi ya Mandela yanalinganishwa na yale ya Papa John Paul II mwaka 2005, ambayo yalihudhuriwa na wafalme watano, malkia sita wa falme mbalimbali na marais wapatao 70 na mawaziri kadhaa, wakiwamo wafuasi wake zaidi ya milioni mbili. Yanakadiriwa pia kulingana na maziko ya Winston Churchil aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza mwaka 1965.
Marais wote wa Marekani walio hai wanatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo iwapo afya zao zitawaruhusu kusafiri, pamoja na Prince Charles wa Uingereza na hata Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe. Pia watu maarufu wenye urafiki wa karibu na Mandela akiwamo msanii Oprah Winfrey wameshathibitisha kuhudhuria.
Changamoto la kiusalama
Kutokana na idadi kubwa ya wakuu wa nchi na watu maarufu duniani wanaotarajiwa kufika Afrika Kusini, suala la usalama limeelezewa kuwa changamoto mpya kwa vyombo vya usalama nchini humo.
Afrika Kusini imekuwa moja ya nchi zinazokabiliwa na matukio ya uporaji na mauaji yanayotokana na idadi kubwa ya wahalifu, wengi wao wakidaiwa kuwa wahamiaji haramu.
“Huyu ni shujaa wa dunia. Tutafanya mipango ya mazishi makubwa ambayo hayajawahi kushuhudiwa. Nadhani kila nchi itakuwa imeandaa utaratibu wake wa namna ya kushiriki,” alisema mmoja wa wanadiplomasia wa Afrika Kusini ambaye hakutaka kutajwa jina lake.
Siku 11 za maombolezo
Serikali ya Afrika Kusini, kwa mujibu wa gazeti la The Guardian tayari imeweka wazi ratiba ya siku 11 za maombolezo tangu alipofariki dunia juzi jioni. Japokuwa ratiba hiyo ilishaandaliwa karibu mwaka mmoja uliopita na kupitiwa na kufanyiwa maboresho katika baadhi ya maeneo, inaonyesha namna maofisa wa Serikali ya Afrika Kusini walivyolipa uzito suala hilo na kulifanya kuwa tukio la kukumbukwa katika historia.
Mwannchi

HII NDIYO KAULI YA MH. ZITTO KUHUSU WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KUTANGAZA MSHAHARA WAKE BILA SHURUTI,


                                                           Picha ya zito kabwe
  • WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA.

    WAZIRI MKUU Mizengo Pinda, amesema mshahara wake kwa mwezi ni sh. milioni sita hivyo watu wanaosema analipwa zaidi ya hizo, wanalengo la kutaka kuharibu jina lake.
     
    Pinda aliyasema hayo bungeni Mjini Dodoma jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo akionesha kushangazwa na watu wanaodai analipwa sh. milioni 30 kwa mwezi. 


    "Hizi ni njama za watu wachache wanaotaka kuharibu jina langu, wanasema najiita Mtoto wa Mkulima wakati nalipwa sh. milioni 30 kwa mwezi si kweli...nalipwa sh. milioni sita tu ambayo ni pamoja na posho," alisema. 



    Akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Ole, Bw. Rajabu Mbarouk Mohammed (CUF), juu ya mchakato wa vitambulisho vya Taifa kukamilika kabla ya Uchaguzi Mkuu 2015, Bw. Pinda alisema hadi sasa mchakato huo unaendelea vizuri. 



    "Pamoja na kuchelewa kwake, Serikali imeweza kujitahidi ili kuhakikisha unakwenda vizuri kwa kuwafikia watu wote," alisema. 



    Katika hatua nyingine, Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda, amewataka wabunge kuacha kutanguliza masilahi ya vyama vyao ndani ya Bunge badala yake watangulize masilahi ya Taifa kwa manufaa ya Watanzania wote. 



    Bi. Makinda aliyasema hayo bungeni Mjini Dodoma jana wakati wa kipindi cha kuchangia Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni Mwaka 2013. 



    "Wabunge mnapaswa kuacha tofauti zenu za kichama ndani ya Bunge ambalo ni chombo muhimu cha kujadili maendeleo ya Taifa na wananchi wake...lipo tatizo la ushabiki wa vyama ndani ya Bunge hasa chama kimoja kinapowasilisha hoja, tunadili kwa pamoja kuijenga nchi yetu," alisema. 



    Akichangia muswada huo, Mbuge wa Maswa Magharibi, mkoani Simiyu, Bw. John Shibuda (CHADEMA), alisema mchakato wa maandalizi ya kura za maoni si mzuri. 



    "Ni muhimu jamii ipewe elimu ya kutosha...kama muswada huu utapita, tuhakikishe vituo vya upigaji kura za maoni vinakuwepo ndani na nje ya nchi ili kutoa fursa kwa Watanzania waishio nje kupiga kura kama wenzao waliopo nchini," alisema. 



    Naye Mbunge wa Mbozi Magharibi, mkoani Mbeya, Bw. David Silinde (CHADEMA), alisema ni vyema Serikali ianze kuboresha daftari la kudumu kabla ya kuanza mchakato huo kwani kuna Watanzania wengi ambao majina yao hayapo katika daftari. 



    Alisema haziungi mkono Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania Bara (NEC) na ile ya Zanzibar ZEC kupewa jukumu la kusimamia mchakato huo badala yake waachiwe wananchi wenye vigezo waombe kusimamia kura za maoni wakiwemo walimu. 



    Muswada huo uliwasilishwa bungeni juzi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera ,Uratibu na Bunge), Bw. William Lukuvi. --

  • -MAJIRA