
Ni
kipindi cha katikati ya wiki hii ambapo tulianza kusikilia kikundi
kinaitwa Panya road ambapo kwa wakazi wa maeneo ya kigogo mpaka
Mburahati na maeneo mengine kama Ilala na Buguruni wamelalamika juu ya
vijana hao ambao wanajikusanya na kutembea pamoja wakiwa zaidi ya 30 na
endapo ukikutana nao wao huchukua pesa au simu za mkononi.

Sasa
kutokana na hali hiyo leo jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam
wameitisha kikao cha makamanda wote wa jiji hili kisha baadae kuitwa
waandishi wa habari kwa ajili ya matukio ambayo yamewahi kufanywa na
vijana hao,kwa sasa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam
limefanya msako na doria katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti makundi
ya uhalifu wa aina mbalimbali.
Makundi hayo ni pamoja na vijana wahuni wasio na kazi maalu maarufu
kwa jina la MBWA MWITU au PANYA ROAD.Maeneo yote ambayo yametajwa
kuonekana vijana hao kama vile Kigogo, Magomeni, Tabata, Manzese na
maeneo ya Mbagala,wamepangwa askari wa kutosha wa doria ili kudhibiti
mlipuko wowote wa vitendo vya kihuni vyenye ishara ya uhalifu
vinanyoleta hofu kwa wananchi.

Kwa
ujumla ni kwamba vijana hao hawana uwezo tena wa kufanya uhalifu katika
makundi yao kutokana na mpango kazi uliopangwa na jeshi la Polisi Kanda
maalum na kwa sasa tayari wamashakamatwa viongozi [Ring Leaders] [06]
wa vikundi hivyo na majina yao ni kama ifuatavyo;
- ATHUMAN SAID Miaka 20 Mkazi wa Kigogo.
- JOSEPH PONELA Dereva Bodaboda,Mkazi wa Kigogo Mkwajuni.
- CLEMENT PETER Miaka 25,Fundi Seremala,Mkazi wa Kigogo.
- ROMAN VITUS Miaka 18,Mfanya biashara Mkazi wa Kigogo.
- MWINSHEHE ADAM Miaka 37, Mkazi wa Temeke Mashine ya Maji.
- DANIEL PETER Miaka 25,Mkazi wa Yombo.
Pamoja na udhibiti wa vijana hao,umezuka mtindo wa watu ambao
hawafahamiki maeneo mbalambali ya jiji la Dar es salaam kwa kutumia
ujumbe mfupi au simu za mkononi ‘sms’ wakieleza uvumi kwamba maeneo yao
yamavamiwa na makundi Mbwa Mwitu au Panya Road,Mtindo huo wa uvumi
umeenea sana maeneo ya Kigogo,Magomeni,Manzese na Tabata.Jeshi la Polisi
linatoa onyo kali kuwa mtindo huo ukome kwani watu hao wanasababisha
hofu kwa wananchi bila sababu na Jeshi la polisi limebaini kuwa hakuna
tukio lolote ambalo limefanyika maeneo hayo au kuripotiwa kituo chochote
cha Polisi katika kipindi cha wiki hii ambapo uvumi uvumi umeenea sana.

Jeshi
la polisi limewatoa hofu wananchi wa Dar es Salaam kwamba si kweli kuna
tishio la vijana hao kama inavyosemekana kwani jeshi la Polisi
limejiimarisha kiulinzi na vijana hao hawana uwezo wa kufanya watakavyo
kama uvumi ulivyoenezwa kimakosa.
Uchunguzi umebaini kwamba chanzo cha uvumi huo ni kwamba tarehe
18/05/2014 na 20/05/2014 palitokea mauaji ya vibaka wawili waliohusishwa
na makundi haya na kwamba kulikuwa na hofu kuwa baada ya mazishi ya
vijana hao vijana wenzao wangeweza kulipiza kisasi ndio maana pakawa na
uvumi wa jumbe mbalimbali zilizoleta hofu.
Mwisho kabisa jeshi la polisi limeomba wananchi wawe watulivu na
waendelee na shughuli zao kama kawaida na waachane na uvumi huo.
0 comments:
Chapisha Maoni